TONTO DIKEH AMTOLEA UVIVU VAN VICKER!!

Tonto Dikeh ni mwigizaji anayetajwa kuwa na vituko kuliko wote Nigeria kwa sasa!


Kkatika hali ya kushangaza, imeripotiwa majuzi tu kuwa amegombana na mwigizaji mwenzake wa kiume Van Vicker!

Walikua kwenye mazoezi ya kuandaa filamu mpya ambapo walionekana kuchuniana, kila mtu kivyake, kulikopelekea mwongozaji wao kuwauliza kulikoni? Baada ya swali hilo, Tonto Dikeh alilipuka kwa hasira na matusi dhidi ya Van Vicker, na akaona haitoshi, akawasha sigara akimpulizia moshi.Vyanzo vya huo udaku vimeeleza kuwa kulikua na kazi ya ziada kumtuliza kwani alidiriki hata kumpiga Van Vicker !! Kilichosababisha yote hayo, hakijabainishwa





Kweli umdhaniaye ndie, sie!! Sikuwahi kuwaza hawa watu wanaweza kukwaruzana kiasi hiki.Van Vicker namtafsiri kama mtu asiyependa shari, sijui ni kwa sababu ya uhusika wake kwenye movie au vinginevyo!! Na huyo Tonto ndo namuwaziaga kama mdada flani asiyependa shari! Pengine kuna siri ya hiyo tafrani.

Comments