MBUNGE JEREMIAH SUMARI HATUNAYE TENA!

Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki wa chama cha CCM Bw. Jeremiah Sumari amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa kipindi kirefu. Marehemu aliwahi kupelekwa nchini India kwa matibabu ya muda mrefu na kurudishwa nchini mpaka mauti ilipomkuta katika hospitali ya Taifa Muhimbili.



Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, na awape nguvu wote waliofikwa na msiba huu mzito.

Comments