SIJUI NINA MIKOSI JAMANI!!!

Mimi ni msichana nia miaka 27.kila mwanaume niliyekutana nae ana matatizo yake, tena kila mpya ninaekutana nae ni afadhali wa zamani! Wa kwanza alikuwa akinitenda makusudi manake tunapanga appointment ya kukutana saa sita lakini ataniweka hadi saa 12 halafu atapiga simu kuwa hatoweza kuniona leo so tupange siku nyingine.ilinichukua muda mpaka kufikia uamuzi wa kuachana nae kwa sababu nilipata ushuhuda wa wanawake alionao zaidi yangu.
Wa pili alikuwa njema kimaisha na kikazi but namwita silent killer! Hakutaka kujiachia hadharani na mimi, hata nyumbani kwake sikupajua, tunakutana tu bar na Guest house tena booking unakuta nimeweka mimi kwa hela yangu na haitorudishwa.
Wa tatu nilimpenda pia tena nilidumu nae miaka nane kwenye relationship, sema alitake advantage ya kutanua na wanawake wengine kwa kuwa nilikuwa nasoma nje ya Tz so tulikuwa tunameet likizo tu, one day nilirudi likizo na inaonekana alijisahau au alifanya kusudi kwa sababu nilikuwa na funguo za nyumbani kwake na alijua nakuja kwake for likizo, nikakuta maua na kadi ya mahaba toka kwa mdada mwingine, nikaamua kuachana nae coz hata majibu niliyopata baada ya kumuuliza hayakuridhisha.
Wa nne, ndo tunakaribia kufikisha mwaka but simwelewi vizuri, ni cha pombe,anapenda kukaa bar na washkaji, na tulikubaliana kutofanya mapenzi mpaka tuoane japo sioni dalili ya yeye kuzungumzia ndoa zaidi ya yeye kuja kwangu mara kwa mara kuliko mimi ninavyopelekwa kwake.Ki ukweli bado namsikilizia japo hajaonyesha dalili za kunikwaza that much na ningependa nitulie nae awe mume wangu Mungu akipenda.
Naombeni ushauri wenu jamani manake najihisi nina mikosi labda!!Asante.

Comments