UNAWEZA KUBADILI FANI YAKO PALE INAPOBIDI NA UNAVYOJISIKIA

Kung`ang`a nia kitu kimoja ambacho pengine hakina faida ni kosa kubwa wengi wetu tunalifanya.Wataalamu wanasema sii vibaya kubadili hata fani yako ukaelekea kwenye fani nyingine ambayo uko comfortable nayo au inakulipa vizuri zaidi, au kutokana na ratiba ambayo unahisi itaathiri kiwango cha fani yako, na ukairejea baada ya muda pale unapojisikia kuendana na wakati wenyewe.
Angalia mfano wa muigizaji huyu wa majuu ambaye aliingiwa na uthubutu wa kutangaza kuacha kuigiza kwa muda ili ajiendeleze kimasomo, japo alishawahi kuwa mwigizaji wa kike anayelipwa hela nyingi kuliko wote Hollywood mwaka 2009.

Anaitwa Emma Watson, aliyefanikiwa kulipwa dola milioni 30 mwaka 2009, na bado akawa na uthubutu wa kutangaza hilo kwa mashabiki wake japo baadaye alirejea ulingoni mpaka sasa yuko vizuri tu.

Comments